DIVISHENI ZA KEIYO, KAPOMBOI KUANZA HUDUMA

Serikali imepania kurahisisha upatikanaji wa huduma zake muhimu kwa wananchi katika kaunti ya Trans Nzoia kupitia kuanzishwa kwa divisheni 2 za Keiyo na Kapomboi na kata ndogo ya Teitei katika eneo bunge la Kwanza kaunti hiyo. Tangazo hilo limewekwa wazi na Waziri wa usalama wa kitaifa Kipchumba Murkomen ambaye pia amesema serikali ina mpango wa […]

CITY WAONYESHWA VIMULIMULI VYA BLUES

Bao la Enzo Fernandez dakika za mwisho ziliipa Chelsea pointi 1 muhimu kwenye sare ya bao 1 na Manchester City na kudidimiza matumaini ya City kushindana na Arsenal katika uwandaji wa taji la ligi kuu ya soka nchini Uingereza EPL. Kiungo wa Uholanzi Tijjan Reijnders aliwaweka City kifua mbele kabla ya kipindi cha kwanza kutamatika […]

CAMEROON WAKATA TIKETI DHIDI YA MOROCCO

Timu ya taifa ya Cameroon itamenyana na wenyeji wa dimba la taifa bingwa barani Afrika AFCON Morocco kwenye robo fainali ya dimba hilo, baada ya kuwalaza Afrika Kusini mabao 2-1 kwenye pambano lililojaa mihemko. Baada ya kuanza kwa kishindo, Afrika Kusini waligutushwa na bao la beki wa Stoke City Junior Tchamadeu katika dakika ya 34 […]

POLISI WAIMARISHA KIKOSI

Mabingwa watetezi wa ligi kuu ya soka nchini KPL Police FC, wamewasajili wachezaji 3 raia wa kigeni ili kuimarisha kikosi chake katikia juhudi za kutetea taji hilo ligi inapoingia katika mkondo wa mwisho. Watatu hao ni Yves Koutiama wa Burkina Faso aliyeshiriki dimba la CHAN mwaka jana hapa nchini, kiungo mwenye uwezo wa kusakata nafasi […]

LEOPARDS WAKATWA KUCHA INGO DERBY

AFC Leopards walipoteza nafasi kileleni mwa jedwali la ligi kuu ya soka nchini KPL, baada ya kupokezwa kichapo cha bao 1-0 na Kakamega Homeboyz uwanjani Nyayo jijini Nairobi. Licha ya kutoshana pointi wakiwa na 24, Homeboyz wanaidunisha Leopards kwa ubora wa mabao, wakirejea kileleni baada ya kupoteza nafasi hiyo mwanzoni mwa msimu. Bao la Henry […]

POLISI WACHUNGUZA MAKABILIANO YA ALAI-BABU

Polisi jijini Nairobi wanaendeleza uchunguzi katika tukio ambapo mbunge wa Embakasi East Babu Owino anadai kushambuliwa na mwakilishi wadi ya Kileleshwa Robert Alai kwenye makabiliano yanayodaiwa kuhusisha tishio la ufyetuaji wa risasi. Kwenye tukio hilo lililofanyika katika eneo moja la burudani mtaani Kilimani, Owino ambaye tayari ameandikisha taarifa na polisi, anadai kushambuliwa na Alai alipokuwa […]

UCHUNGUZI WA JUMBA SOUTH C WAENDELEA

Uchunguzi katika jengo lililoporomoka mtaani South C mwishoni mwa wiki jana umeshika kasi, mkurugenzi wa mashtaka ya umma Renson Ingonga sasa akimtaka Inspekta mkuu wa polisi Douglas Kanja kuandikisha taarifa ya mwanakandarasi aliyekuwa akijenga jengo hilo na maafisa wote waliohusika katika uidhinishaji. Kupitia taarifa, Ingonga amesema faili ya uchunguzi itatoa mwelekeo kuhusu hatua zitakazochukuliwa dhidi […]

GACHAGUA AITAKA MAREKANI ‘KUCHEZA KIVENEZUELA’

Aliyekuwa naibu rais Rigathi Gachagua ametoa wito kwa serikali ya Marekani kuharakisha uchunguzi unaoendelea katika Sakata ya ulaghai kupitia mpango wa kuwasaidia Watoto wasiojiweza katika jimbo la Minnesota, akisema sehemu ya mapato ya ulaghai huo ilifadhili kampeni za Rais William Ruto kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka wa 2022. Gachagua ameitaka Marekani kuwafuatilia wahusika, akidai baadhi […]

RUTO AAGIZA BUNDUKI HARAMU ZISALIMISHWE

Rais William Ruto kwa mara nyingine amewaonya wamiliki wa bunduki haramu katika eneo la Kerio Valley kuziwasilisha mara moja kwa maafisa wa usalama akionya kuwa watakaokiuka watakabiliwa kisheria. Rais alikuwa akizungumza katika kaunti ya West Pokot, akipongeza operesheni ya kuwakabili majangili eneo hilo la Kerio. Imetayarishwa na Antony Nyongesa

9 WAFARIKI KWENYE AJALI NAIVASHA

Watu 9 wakiwemo Watoto wameaga dunia kwenye ajali ya barabarani kwenye barabara na Nakuru- Nairobi karibu na eneo la Kayole Naivasha baada ya basi la uchukuzi kugongana na gari dogo la uchukuzi aina ya Nissan. Afisa wa idara ya upelelezi eneo hilo Isaac Kiama, amethibitisha ajali hiyo ya mapema leo, akisema mansura wanatibiwa katika hospitali […]