#Local News

LSK YASISITIZA KUENDELEZA MGOMO WAO

Chama cha Wanasheria nchini, LSK, kimethibitisha kuwa mgomo wake wa kutoshiriki katika shughuli za mahakama bado unaendelea kote nchini, huku kikitoa wito kwa mawakili wote kuendelea kususia vikao vya mahakama ili kushinikiza uwajibikaji zaidi ndani ya Idara ya Mahakama.

Akizungumza hii leo nje ya Mahakama ya Juu, Rais wa LSK, Charles Kanjama, amesema mgomo huo unaendelea kuzingatiwa katika maeneo mbalimbali nchini na kuwahimiza wanachama wote kuendelea kutekeleza agizo hilo.

Imetayarishwa na Hilda Ajema

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *