AKONNOR ATAKA KIKOSI CHA GOR KUJITUMA ZAIDI
Kocha wa Gor Mahia Charles Akonnor anaamini kuwa kichapo cha timu yake cha mabao 2-0 dhidi ya Rayon Sports ya Rwanda ni funzo kubwa kwa timu yake kulekea msimu mpya wa ligi.
Kocha huyo Raia wa Ghana amesema kichapo hicho kimempa mtazamo zaidi katika maeneo yanayostahili kuimariswa kikosini wakati Gor Ikijiandaa kutetea taji la ligi kuu humu nchini pamoja na mashindano ya klabu bingwa barani Afrika.
Akonnor amesema kuwa mchezo huo sio taswira kamili ya jinsi kikosi chake kitakavyokuwa msimu ukiendelea.
Imetayarishwa na Cyrus Sifuna
English 































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































