#Local News

JAJI MKUU KOOME ATAKA MATUMIZI YA UJASUSI KUKABILI UHUNI

Jaji Mkuu Martha Koome amesema vitendo vya uhuni vinaweza kuzidi uwezo wa polisi kukusanya ushahidi na kuwafikisha wahusika mahakamani, hasa vinapohusisha makundi makubwa ya watu.

Koome amesema ni muhimu kwa vyombo vya usalama kutumia mbinu za kijasusi pamoja na mikakati mingine ya mapema ili kuwabaini wahusika na kuzuia matukio hayo kabla hayajatokea.

Aidha, amesisitiza kuwa hatua za kuzuia uhalifu mapema ni muhimu katika kuimarisha usalama wa wananchi na kuhakikisha wahalifu wanawajibishwa kwa mujibu wa sheria.

Imetayarishwa na Cyrus Sifuna

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *