MGOMO WA WAHUDUMU WA AFYA WAANZA NCHINI
Huduma za afya nchini zimeathirika baada ya maelfu ya wahudumu wa afya chini ya Muungano wa Vyama vya Afya kuanza mgomo wa kitaifa hapo jana
Mgomo huo umeanza kufuatia kumalizika kwa notisi ya siku 14 iliyotolewa Julai 6, baada ya mazungumzo kati ya vyama vya wafanyakazi, serikali ya kitaifa na serikali za kaunti kutofikia mwafaka kuhusu masuala ya kikazi.
Hatua hiyo inatarajiwa kuvuruga utoaji wa huduma katika hospitali nyingi za umma huku wahudumu wakisisitiza kuwa hawatarejea kazini hadi malalamishi yao yatakaposhughulikiwa.
Imetayarishwa na Cyrus Sifuna
English 































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































