MABADILIKO YA TABIA NCHI YAATHIRI ELIMU YA WATOTO BARANI AFRIKA
Watoto milioni mia moja kumi na nane hawaendi shuleni kutokana na migogoro na dharura za mabadiliko ya tabia nchi katika bara la Afrika.
Waziri mkuu wa mawaziri Musalia mudavadi amesema kando na watoto hao mamilioni ya watu wamelazimika kuhama makazi yao kutokana na changamoto za usalama katika mataifa ya bara hili.
Mudavadi amerai taasisi za kidini zikiongozwa na kanisa kuwa mustari wa mbele kutetea ulindaji wa haki za kibinadamu katikati ya migogoro hii.
Imetayarishwa na Hilda Ajema
English 































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































