SEKTA YA USAFIRI WA ANGA YAKABILIWA NA TISHIO LA MGOMO
Sekta ya usafiri wa anga nchini inakabiliwa na tishio la mgomo baada ya Muungano wa Wafanyakazi wa Usafiri wa Anga Kenya (KAWU) kutoa ilani ya siku saba ya kusitisha kazi.
Mgomo huo unatarajiwa kuwaathiri wafanyakazi wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Kenya (KCAA), Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Kenya (KAA), Kenya Airways na Jambojet.
Muungano huo umesema uamuzi huo umechochewa na migogoro ya muda mrefu ya kikazi, ikiwemo kucheleweshwa kwa utekelezaji wa mikataba ya pamoja ya wafanyakazi pamoja na wasiwasi kuhusu usalama wa ajira.
Imetayarishwa na Cyrus Sifuna
English 































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































