MURKOMEN: DCI INACHUNGUZA MASHAMBULIZI YA OL KALOU
Waziri wa usalama wa ndani Kipchumba Murkomen amesema Idara ya Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI) imeanzisha uchunguzi kuhusu watu wanaodaiwa kuwashambulia wapigakura na wanahabari wakati wa uchaguzi mdogo wa Ol Kalou.
Murkomen amesema wote watakaobainika kuhusika na matukio hayo watachukuliwa hatua kali za kisheria, akionya wanasiasa dhidi ya kuajiri wahuni kuvuruga shughuli za kisiasa.
Aidha, amesisitiza kuwa si wahusika pekee watakaokamatwa, bali pia wale watakaobainika kufadhili au kupanga mashambulizi hayo watafikishwa mbele ya sheria.
Imetayarishwa na Cyrus Sifuna
English 































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































