NTSA YAWAKAMATA WATU 45 KWA KOSA LA KUTOTUMIA KIVUKIO KATIKA ENEO LA NYAYO
Mamlaka ya Kitaifa ya Uchukuzi na Usalama Barabarani NTSA imewakamata watu 45 kwa kuvuka barabara badala ya kutumia kivukio cha daraja katika eneo la Uwanja wa Nyayo jijini Nairobi.
NTSA imesema kuwa watu hao watashtakiwa kwa mujibu wa Sheria ya Trafiki kwa kuvuka barabara katika maeneo yasiyoruhusiwa.
Mamlaka hiyo imeeleza kuwa operesheni hiyo ni sehemu ya juhudi za kuimarisha usalama barabarani na kupunguza idadi ya vifo vya watu wanaotembea kwa miguu.
Imetayarishwa na Hilda Ajema
English 































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































