WATU 5 WAFARIKI BAADA YA KUPOROMOKEWA NA MGODI TRANSMARA
Watu watano wamethibitishwa kufariki dunia baada ya mgodi kuporomoka katika eneo la Lolgorian, Transmara Kusini, Kaunti ya Narok.
Naibu Kamishna wa Kaunti Ndogo hiyo ya Transmara Stephen Odeke, amesema juhudi za uokoaji bado zinaendelea, licha ya kutatizika kutokana na ukosefu wa vifaa maalumu vinavyohitajika .
Kulingana na Odeke idadi kamili ya wachimbaji waliokwama chini ya mgodi huo bado haijafahamika, huku ikiaminika kuwa watu kadhaa bado wamenaswa ndani ya mgodi huo.
Imetayarishwa na Hilda Ajema
English 































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































