#Local News

DUALE: HAKUNA WAGENI WALIOWEKWA KARANTINI LAIKIPIA

Waziri wa Afya Aden Duale amekanusha taarifa kwamba wahudumu saba wa misaada kutoka Marekani wamewekwa karantini katika kituo cha Ebola kinachofadhiliwa na Marekani katika Kituo cha Jeshi la Anga cha Laikipia.

Duale amesema serikali ilisimamisha ujenzi wa kituo hicho baada ya mahakama kutoa amri ya kusitisha mradi huo, hivyo taarifa hizo si za kweli.

Aidha, amesema serikali haitafichua maeneo ya vituo vya karantini na kutenga wagonjwa wa Ebola, akieleza kuwa kufanya hivyo kunaweza kuwakatisha tamaa wananchi kutafuta huduma za matibabu wanapohitaji.

Imetayarishwa na Cyrus Sifuna

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *