#Local News

MARTHA KOOME AMFUTA KAZI HAKIMU MMOJA KWA TUHUMA ZA HONGO

Jaji mkuu martha koome amemsimamisha kazi hakimu mmoja baada ya kukamatwa na tume ya maadili na kukabiliana na ufisadi EACC,kwa tuhuma za kupokea na kuomba hongo kuhusiana na kesi iliyokuwa mahakamani.

EACC inasema hakimu huyo pamoja na afisa wa uangalizi walikamatwa wakipokea hongo ya shilingi elfu 150 ili kuhakikisha mshtakiwa anapata adhabu isiyo ya kifungo.

Jaji koome amesema idara ya mahakama ina sera ya kutovumilia ufisadi huku taratibu za kinidhamu zikianza mara moja.

Imetayarishwa na Hilda Ajema

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *