MMOJA WA MASHAHIDI AZUNGUMZA KUUWAWA KWA ALBERT OJWANG
Mmoja wa mashahidi katika kesi ya marahemu Albert Ojwang mwanaume aliyedaiwa kuuwawa kwenye seli ya kituo cha polisi cha Nairobi Central ameiambia mahakama ya Kibra kuwa aliagizwa kufuta picha za kamera za CCTV zilizorekodi matukio ya tarehe 6 na tarehe 7 Juni mwaka wa 2025.
Akitoa ushahidi katika kesi ya kifo cha Ojwang shahidi huyo amesema aliwaelekeza waliohusika kuwa haingewezekana kufuta rekodi za siku hizo pekee badala yake aliamua kuifuta data yote kwenye hifadhi data yaani hard disk iliyokuwa imehifadhi data hizo.
Imetayarishwa na Hilda Ajema
English 































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































