KARAURI ATANGAZA AZMA YA KUGOMBEA UGAVANA NAIROBI
Mbunge wa Kasarani, Ronald Karauri, ametangaza rasmi azma yake ya kuwania kiti cha ugavana wa Nairobi katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2027.
Akizungumza katika mkutano ulioongozwa na Rais William Ruto katika Ikulu,Karauri alitetea mpango wa Nyumba za Bei Nafuu, akisema umetoa ajira na kuboresha maisha ya wananchi wengi.
Aidha, alimkosoa Seneta wa Nairobi Edwin Sifuna kwa kauli zake kuhusu mpango huo, akisisitiza kuwa utekelezaji wa mradi huo umeleta manufaa kwa mafundi na wakazi wengi wa jiji.
Imetayarishwa na Cyrus Sifuna
English 































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































