KINDIKI APUUZA MATOKEO YA UCHAGUZI WA OL KALOU
Naibu Rais Profesa Kithure Kindiki ameongoza viongozi wa Kenya Kwanza kupuuza ushindi wa upinzani katika uchaguzi mdogo wa ubunge wa Ol Kalou, akisema matokeo hayo hayana athari kwa maandalizi ya uchaguzi mkuu ujao.
Akizungumza mjini Embu Kindiki amesema Rais William Ruto bado yuko katika nafasi nzuri ya kutetea kiti chake na kupata muhula mwingine wa uongozi.
Aidha, amewataka viongozi wa eneo la Mlima Kenya kuendelea kushirikiana na kudumisha umoja, akisisitiza kuwa mshikamano utachangia maendeleo ya eneo hilo na taifa kwa ujumla.
Imetayarishwa na Cyrus Sifuna
English 































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































