#Basketball #Sports

BASKETBALL: KPA YALENGA KUIMARISHA SAFU YA  ULINZI LICHA YA MATOKEO MAZURI

Kocha wa Kenya Ports Authority (KPA), Robert Mugabe, amesema timu yake itaendelea kuboresha safu ya ulinzi licha ya kupata ushindi mara mbili mfululizo katika Ligi Kuu ya Mpira wa Kikapu kwa Wanaume.

KPA iliichapa Moischers kwa alama 88-57 kabla ya kuifunga ANU Wolfpacks kwa 89-70, katika mechi zilizochezwa mwishoni mwa wiki katika viwanja vya USIU.

Mugabe amesema safu ya ushambuliaji inaonyesha maendeleo mazuri kwa kutengeneza nafasi nyingi za kufunga, lakini amesisitiza kuwa kipaumbele sasa ni kuimarisha ulinzi kuelekea mechi zijazo.

Imetayarishwa na Cyrus Sifuna

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *