#Local News

NYAMITA: USHINDI WA OL KALOU SIO KIPIMO CHA URAIS

Mbunge wa Uriri, Mark Nyamita, amesema upinzani unasherehekea ushindi wa uchaguzi mdogo wa Ol Kalou kupita kiasi, akidai kuwa ni ushindi mmoja tu ambao hauwezi kuamua mwelekeo wa siasa za kitaifa.

Nyamita amesema uchaguzi huo umeonyesha kuwa hakuna muungano wa kweli wa upinzani, akieleza kuwa vyama vya upinzani vilishindwa kusimamisha mgombea mmoja kama ishara ya umoja wao.

Aidha, amesisitiza kuwa matokeo ya Ol Kalou hayana uhusiano na uchaguzi wa urais, akibainisha kuwa Rais William Ruto hakuwa mgombea katika uchaguzi huo.

Imetayarishwa na Cyrus Sifuna

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *