#Local News

ORERO ATAKA HATUA KALI DHIDI YA WAHUNI

Mbunge wa Kibra Peter Orero amemtaka Inspekta Jenerali wa Polisi Douglas Kanja kuchukua hatua madhubuti kukabiliana na ongezeko la vitendo vya uhuni vinavyoshuhudiwa katika shughuli za kisiasa.

Mbunge huyo pia amewataka wanasiasa kuacha kutumia wahuni kutekeleza malengo yao ya kisiasa, akisema tabia hiyo inachochea vurugu na kuhatarisha usalama wa wananchi.

Aidha, ameonya kuwa ikiwa hatua za haraka hazitachukuliwa, nchi inaweza kuelekea katika hali ya kutotii sheria, hasa wakati taifa linapojiandaa kwa uchaguzi mkuu ujao.

Imetayarishwa na Cyrus Sifuna

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *