NYAOKE APIGIA UPATO KIKOSI CHAKE KUSHINDA TAJI LA CECAF
Kocha mkuu wa timu ya taifa ya Kenya soka la walemavu kwa wanawake Sharon Nyaoke anasadiki kwamba wachezaji wake wanaweza kushinda taji la CECAAF litakaloandaliwa mjini Bujumbura, Burundi mwezi Septemba.
Timu hiyo itashiriki CECAAF kwa mara ya kwanza na wamedhamiria kuwabwaga wapinzani wao, baada ya kuibuka wanne katika Kombe la Dunia mwaka jana nyuma ya mabingwa na wenyeji Colombia, Marekani na Poland.
Nyaoke hata hivyo anataka uungwaji mkono zaidi kutoka kwa serikali wanapojiandaa kwa mashindano hayo.
Imetayrishwa na Nelson Andati
English 































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































