IPOA: 65 WALIUAWA KWENYE MAANDAMANO
Watu 65 waliuawa kutokana na maandamano yaliyoshudiwa katika miezi ya Juni na Julai mwaka huu pekee.
Haya ni kwa mujibu wa ripoti ya mamlaka ya kutathmini utendakazi wa polisi IPOA, ambayo pia imewalaumu polisi kwa madai ya kutumia nguvu kupita kiasi.
Miongoni mwa walioangamia ni Victor Otieno kutoka Bungoma, mwanafunzi aliyepigwa risasi katika eneo la Juja ambaye familia yake imeilaumu IPOA kwa misingi ya kujikokota katika uchunguzi.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































