MACHIFU MANDERA KUPEWA BUNDUKI, MURKOMEN
Serikali imetoa hakikisho la usalama katika eneo la Border One kwenye mpaka wa Kenya na Somalia baada ya kuibuka hofu mapema mwezi huu kuhusu uwepo wa vikosi vya wanajeshi wa Jubaland nchini Somalia.
Akizungumza alipozuru kaunti ya Mandera, Waziri wa usalama wa kitaifa Kipchumba Murkomen, amesema usalama wa ndani umerejeshwa na kwamba machafuko kwenye mataifa Jirani hayataathiri usalama nchini.
Amefichua kuwa machifu katika kaunti ya Mandera watapewa bunduki ili kuwalinda wananchi.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































