KNCHR YAONYA KUHUSU KEJELI
Tume ya kitaifa kuhusu haki za kibinadamu KNCHR imewaonya wakenya dhidi ya kuwakejeli watu walio na changamoto za kimaumbile ikiwemo kwenye mitandao ya kijamii, kwamba hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yao.
Kulingana na tume hiyo, watakaopatikana na hatia hiyo watatozwa faini ya shilingi milioni 1 au kifungo kischozidi mwaka mmoja au yote mawili.
Onyo ya KNCHR imejiri kufuatia tukio ambao mtu aliye na changamoto za kimaumbile alidhalilishwa mitandaoni maajuzi, tume hiyo ikisema hatua hiyo ni ukiukaji wa katiba na sheria zinawalinda.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































