FAMILIA ZAACHIWA KUWASAKA WAPENDWA WAO
Shughuli za kuwasaka watu 10 wanaohofiwa kukwama kwenye udongo kufuatia maporomoko ya ardhi katika eneo la Chesongoch kaunti ya Elgeyo Marakwet zinaendelea huku serikali ikiratibu tarehe 21 mwezi huu kuwa siku ya kuwazika walioangamia.
Shughuli hizo zinaendelezwa na familia za waathiriwa na Wakazi, baada ya maafisa wa serikali kuondoka ikiwa ni wiki moja tangu kutokea kwa mkasa huo.
Watu 38 wamethibitishwa kufariki huku wengine 10 wakiwa hawajulikani waliko.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 






























































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































