WASHUKIWA 7 WA VURUGU KARIOBANGI WAKAMATWA
Idara ya polisi imethibitisha kuwakamata watu 7 wanaohusishwa na vurugu zilizoshuhudiwa katika kanisa moja mtaani Kariobangi North jijini Nairobi wakati wa ibada iliyokuwa ikihudhuriwa na aliyekuwa naibu rais Rigathi Gachagua.
Kupitia taarifa, idara hiyo imesema washukiwa Charles Opiyo, Wilson Okoth, Michael Mutunga, Reggy Opiyo, Brian Omondi, Gordon Onyango na Elisha Ochieng wamekamatwa mtaani Lucky Summer.
Uchunguzi katika vurugu hizo unaendeshwa na kamanda wa polisi eneo la Nairobi na mkurugenzi wa idara ya upelelezi wa jinai DCI.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































