MASWALI KUHUSU KIFO CHA JIRONGO
Familia ya mfanyabiashara na mwanasiasa tajika Cyrus Jirongo, imeshinikiza majibu kuhusu utata unaozingira kifo cha mfanyabiashara huyo kwenye ajali siku ya Ijumaa usiku, polisi wakisema Jirongo alikuwa akielekea Nairobi kwenye gari lake wakati wa ajali hiyo.
Hata hivyo, kulingana na mwenyekiti wa kamati ya mipango ya mazishi Fred Gumo na aliyekuwa seneta wa Vihiga George Khaniri, Jirongo alikuwa katika eneo la Karen majira ya saa 5 usiku, kabla ya ajali yake kuripotiwa takribani dakika 30 baadaye eneo la Naivasha.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































