RUTO ATANGAZA SERA YA KUWALINDA “WACHACHE”
Kenya imejiunga na ulimwengu kuadhimisha siku ya jamii za watu wachache, rais William Ruto akitangaza kuidhinishwa kwa sera itakayotetea haki za jamii hizo.
Akizungumza kwenye kikao na jamii hizo kinacheoendelea katika Ikulu ya Nairobi, Ruto ameahidi kuwa sera hiyo iliyoidhinishwa na baraza la mawaziri, itafanikisha vita dhidi ya dhuluma dhidi ya jamii hizo ikiwemo umiliki wa mashamba na nafasi za ajira katika ngazi zote za serikali.
Sera hiyo itahitaji mkono wa bunge kabla ya kuwa sheria.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































