OMOLLO AONYA VIONGOZI DHIDI YA KUCHOCHEA GHASIA MIGORI
Katibu Mkuu wa Wizara ya Usalama wa Ndani, Raymond Omollo, ameonya viongozi wa kisiasa katika Kaunti ya Migori na maeneo mengine nchini dhidi ya kuwatumia vijana kuchochea ghasia.
Akizungumza katika eneo la Suna Magharibi Omollo amesema serikali haitaruhusu wanasiasa kutumia vurugu kuwatisha wapinzani au kuvuruga shughuli za kisiasa.
Omollo aidha amewataka viongozi wa Migori kukumbatia siasa za amani, akionya kuwa kaunti hiyo haipaswi kurudishwa katika migogoro kama ilivyoshuhudiwa wiki za karibuni.
Imetayarishwa na Cyrus Sifuna
English 































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































