#Local News

MVUA KUBWA KUANZA ALHAMISI

Wakenya wametahadharishwa kuhusu viwango vya juu vya mvua katika baadhi ya maeneo tya nchi kuanzia hapo kesho, idara ya utabiri wa hali ya anga ikisema mvua hiyo itanyesha kwa vipindi.

Kwa mujibu wa utabiri wake, nyanda za juu za magharibi na mashariki mwa bonde la ufa, ukanda wa Ziwa Victoria, nyanda za chini za Mashariki mwa nchi na ukanda wa pwani yatashuhudia mvua.

Idara hiyo imeonya kuhusu uwezekano wa mvua kusababisha mafuriko katika baadhi ya maeneo hayo na kuwataka wakazi kuchukua tahadhari.

Imetayarishwa na Antony Nyongesa

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *