SIFUNA ABADILISHA WIMBO ASEMA HAWEZI KUWA ‘SG’ WA ODM
Seneta wa Nairobi Edwin Sifuna sasa ameonekana kubadilisha maneno yake na kusema kuwa hawezi kuwa katibu mkuu wa chama hicho kwa sasa.
Kauli ya Sifuna inakuja siku moja baada ya mahakama kutupilia mbali kesi yake ya kutolewa kama Katibu mkuu wa Chama hicho na kutaka suluhu la ndani ya chama.
Sifuna sasa ameonekana kuwachilia nafasi hiyo wakati wa mkutano wa Kundi la Linda Mwananchi katika ukumbi wa Ufungamano.
Imetayarishwa na Cyrus Sifuna
English 
































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































