BANDARI FC YATULIZA TAHARUKI BAADA YA KISA KASARANI
Klabu ya Bandari FC imejitokeza kutuliza hali kufuatia tukio la mvutano lililoshuhudiwa katika mechi yao dhidi ya Gor Mahia uwanjani Kasarani mwishoni mwa wiki
Kocha mkuu Bernard Mwalala amekiri kuwa mwitikio wa wachezaji wake baada ya uamuzi tata wa penalti haukuwa wa kawaida akisisitiza kuwa nidhamu na heshima ni misingi muhimu ya klabu hiyo
Mwalala amesema alilazimika kuingilia kati wakati wa tukio hilo ili kupunguza mvutano na kurejesha utulivu huku akiahidi kuwa hali kama hiyo haitajirudia tena.
Imetayarishwa na Cyrus Sifuna
English 































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































