MWAMUZI ANTHONY TAYLOR ASTAAFU
Mwamuzi wa Ligi Kuu ya Uingereza na Kombe la Dunia, Anthony Taylor, ametangaza kustaafu uamuzi baada ya kuhudumu kwa miaka 20, akitaja shinikizo na ukosoaji mkubwa unaowakabili waamuzi kuwa miongoni mwa sababu za uamuzi wake.
Taylor mwenye umri wa miaka 47 ameongoza jumla ya mechi 831, zikiwemo 432 za Ligi Kuu ya England, na kujijengea sifa kama mmoja wa waamuzi mashuhuri duniani.
Mchezo wake wa mwisho ulikuwa katika Kombe la Dunia ambapo Uhispania iliifunga Ureno bao 1-0, akihitimisha rasmi safari yake ndefu ya uamuzi.
Imetayarishwa na Cyrus Sifuna
English 































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































