WIZARA YA AFYA YATHIBITISHA KISA CHA TANO CHA MPOX NCHINI KENYA
Kenya imethibitisha kisa chake cha tano cha Mpox kinachomhusisha mwanamke mwenye umri wa miaka 29 anayeishi karibu na Chuo cha Tumaini huko Mombasa.
Katika taarifa, Waziri wa Afya Deborah Barasa ameeleza kuwa mwanamke huyo alipata virusi hivyo kutoka kwa mwenziwe, ambaye alikuwa kisa cha nne kuthibitishwa nchini na kwa sasa amelazwa hosipitali.
Mwanamke huyo amelazwa katika Hospitali Kuu ya Pwani baada ya vipimo kubadilika, alitengwa katika Kituo cha Kutengwa cha Hospitali ya Utange cha Mpox.
Imetayarishwa na Janice Marete
English 































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































