#Football #Sports

MOMBASA UNITED WATOKA SARE YA 1-1.3K FC

Timu ya 3K FC kutoka Embu ililazimishwa sare ya 1-1 na Mombasa United katika mechi ya Ligi Kuu ya Taifa iliyochezwa Jana alasiri kwenye Uwanja wa Serani, jijini Mombasa.

Glen Githinji alifunga kwa niaba ya 3K, huku mchezaji wa zamani wa Bandari FC, Wilberforce Lugogo, akifunga bao la kusawazisha kwa Mombasa United.

Akizungumza baada ya mechi, kocha wa Mombasa United, Hamadi Said, alielezea shukrani licha ya kushindwa kushinda nyumbani. Kocha wa 3K, Francis Chege, alilaumu waamuzi kwa kupewa penati anayoita kuwa ya kijinga dhidi yao.

Kutokana na matokeo hayo, 3K sasa wanashika nafasi ya nne kwa pointi 19 kutoka mechi 11, huku Mombasa United wakishika nafasi ya 12. Katika matokeo mengine, Nairobi United walitoka sare ya 1-1 na Samwest FC, Migori ilishinda Dimba Patriots 1-0, Luanda Villa ilishinda 1-2 dhidi ya SS Assad, Fortune Sacco ilitoka sare ya 1-1 na Kibera, huku Kisumu All-Stars wakiibuka na ushindi wa 3-1 dhidi ya MOFA.

Imetayarishwa na Janice Marete

MOMBASA UNITED WATOKA SARE YA 1-1.3K FC

SHAHADA YA KIFO JUU YA MAPENZI

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *