#Football #Sports

REAL MADRID WAMNASA DIOMANDE KWA ZAIDI YA EURO MILIONI 100

Real Madrid imefikia makubaliano na RB Leipzig ya kumsajili winga wa Ivory Coast, Yan Diomande, kwa ada inayozidi euro milioni 100.

Diomande anatarajiwa kusafiri kuelekea Madrid wiki hii kwa ajili ya vipimo vya afya na kukamilisha utiaji saini wa mkataba utakaomuweka katika klabu hiyo hadi Juni 2031.

Usajili huo unatarajiwa kuimarisha safu ya ushambuliaji ya Real Madrid, huku Diomande akionekana kuwa mmoja wa wachezaji wenye mustakabali mkubwa katika soka la Ulaya.

Imetayarishwa na Cyrus Sifuna

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *