#uncategorized

VIONGOZI WA ODM WAMTAKA OPARANYA AWE NAIBU RAIS

Baadhi ya viongozi wa ODM wamekitaka chama hicho kuhakikisha kinapata nafasi ya Naibu Rais katika mazungumzo yake ya kisiasa na UDA, huku wakimuunga mkono Waziri wa Vyama vya Ushirika Wycliffe Oparanya kuwa mgombea mwenza wa Rais William Ruto katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2027.

Wakizungumza katika eneo la Malava, Kaunti ya Kakamega, viongozi hao wamesema uungwaji mkono wa ODM kwa azma ya Rais Ruto ya kutetea urais utategemea chama hicho kupata nafasi ya Naibu Rais.

Imetayarishwa na Cyrus Sifuna

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *