KIAMBU YAWATIMUA MADAKTARI
Mgomo wa madaktari katika kaunti ya Kiambu umechukua mkondo tofauti, baada ya serikali ya kaunti hiyo kuwafuta idadi ya madaktari isiyojulikana kwa madai ya kuhatarisha Maisha ya wagonjwa.
Tangazo la kuwafuta madaktari hao walioanza mgomo hapo jana limewekwa wazi na waziri wa afya kwenye serikali ya kaunti hiyo Elias Maina, zoezi la kuwahesabu madaktari ili kubaini ambao hawajaripoti kazini likiendelea.
Ameongeza kuwa serikali haitakubali sekta ya afya anayosema hupokea shilingi bilioni 8 kila mwaka kulemazwa
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 











































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































