KAUNTI ZAHIMIZWA KUWASILISHA PENSHENI YA WAFANYAKAZI
Katika juhudi za kuwaepushia mahangaiko wafanyakazi wa kaunti wanaostaafu, serikali za kaunti zimehimizwa kuwasilisha malipo ya pensheni kwa hazina ya pensheni ya serikali ili kuwawezesha wafanyakazi hao kujitegemea baada ya kustaafu.
Akizungumza kwenye mkutano wa kitaifa wa hazina hiyo, katibu wa muungano wa wafanyakazi wa kaunti Roba Duba, amesema hadi sasa muungano huo unazidai kaunti zaidi ya shilingi bilioni 30.
Kauli yake ikungwa mkono na naibu msimamizi wa hazina ya pensheni ya kaunti Joseph Rono.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 












































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































