SHA KUGHARAMIA WAHUDUMU WA AFYA
Serikali kuu na zile za kaunti zimekubaliana kuwalipia wahudumu wakujitolea wa afya malipo ya sha bila na kuwakata chochote kwenye malipo yao kuanzia mwaka ujao.
kwa mujibu wa waziri wa afya Aden Duale, ngazi zote mbili za serikali zinatarajiwa kutoa pesa nusu kwa nusu na kugharamia matibabu kamili ya wahudumu hawa wa afya wa nyanjani kwa mradi ambao utagharimu takriban shilingi milioni 9.
Imetayarishwa na Jones Koikai
English 












































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































