#Local News

WANAOUNGA MKONO SERIKALI JUMUISHI WAONGEZEKA

Uungwaji mkono wa serikali jumuishi kati ya ODM na UDA uliongezeka maradufu katika kipindi cha miezi 6 iliyopita, ukipanda kutoka asilimia 22 mwezi Mei hadi asilimia 44 kufikia mwezi Novemba mwaka huu.

Haya nu kulingana na utafiti wa shirika la TIFA, uliolenga kupata maoni kuhusu ushirikiano wa kisiasa kati ya Rais William Ruto na aliyekuwa kinara wa ODM Raila Odinga.

Kwenye utafiti huo, idadi ya wanaopinga ushirikiano huo imeshuka kutoka asilimia 64 mwezi Agosti hadi asilimia 48 mwezi jana.

Imetayarishwa na Antony Nyongesa

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *