POLISI WASHUTUMIWA KWA MAUAJI EMBU
Gavana wa Embu Cecil Mbarire, ameshinikiza uchunguzi huru katika tukio ambapo maafisa wa polisi wanaripotiwa kuwaua watu 3 kwa kuwafyatulia risasi na kuwajeruhi wengine kadhaa wakati wa maandamano katika eneo la Ishiara, Mbeere North.
Wakazi wamesema polisi walitumia nguvu kupita kiasi kudhibiti maandamano hayo ya hapo jana yaliyolenga kushinikiza utendakazi bora katika hospitali ya Ishiara Level 4.
Kupitia taarifa, amesema serikali yake imeanzisha mchakato wa kuangazia masuala yaliyoibuliwa kuhusu hospitali hiyo.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 












































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































