UTULIVU WAREJEA MAJENGO NAIROBI
Utulivu umeanza kureja katika eneo la Majengo karibu na soko la Gikomba jijini Nairobi kufuatia makabiliano mapema leo kati ya polisi na kundi la vijana lililozua vurugu kulalamikia mauaji ya kijana mmoja, wanayesema alipigwa risasi na polisi wa kituo cha California kufuatia tofauti kati ya polisi na kundi la watu wanaosemekana kuwa wauzaji wa mihadarati.
Gari la polisi na afisi ya chifu ni miongoni mwa mali ambayo imeteketezwa kwenye vurugu hizo, vijana hao wakiibua madai kwamba wamekuwa wakidhulumiwa na polisi mara kwa mara.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 












































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































