#Local News

RUKU: SERIKALI INAHITAJI SHILINGI BILIONI 10 KUKABILI UHABA WA CHAKULA

Waziri wa Utumishi wa Umma Geoffrey Ruku, amesema serikali inahitaji takriban shilingi bilioni 10 ili kusaidia wananchi wanaokabiliwa na athari za uhaba wa chakula.

Ruku amesema fedha hizo hazijatengwa katika bajeti ya sasa, hali ambayo imeelezwa kuwa changamoto kubwa kwa serikali katika juhudi za kudhibiti athari za kupanda kwa bei ya vyakula.

Aidha, amesema matumizi ya fedha za ziada kugharamia mipango ya kupunguza gharama za chakula yanaongeza mzigo kwa uchumi wa nchi, licha ya umuhimu wake katika kuwakinga wananchi dhidi ya mfumuko wa bei.

Imetayarishwa na Cyrus Sifuna

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *