#Athletics #Sports

SEREM AILETEA KENYA DHAHABU YA KWANZA MICHEZO YA JUMUIYA YA MADOLA

Edmund Serem ameiletea Kenya medali yake ya kwanza ya dhahabu katika Michezo ya Jumuiya ya Madola 2026 baada ya kushinda mbio za kuruka viunzi na maji za mita 3,000 mjini Glasgow, nchini Scotland.

Serem alimaliza mbio hizo kwa muda wa dakika 8:18.23, akifuatiwa na Simon Koech, aliyeshinda medali ya fedha kwa muda wa dakika 8:18.59, huku Leonard Bett akitwaa medali ya shaba kwa muda wa dakika 8:21.63.

Kenya ilitawala mbio hizo kwa kutwaa nafasi zote tatu za kwanza, na hivyo kuandika historia ya ushindi kamili katika fainali ya mbio za mita 3,000 kuruka viunzi na maji.

Imetayarishwa na Cyrus Sifuna

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *