MAAFISA WA NAIROBI HOSPITAL MAHAKAMANI
Maafisa kadhaa wa Nairobi Hospital wamefikishwa katika mahakama ya Milimani baada ya kukamatwa katika njia tatanishi kuhusiana na makosa ambayo hayajawekwa wazi.
Maafisa hao ni mshauri wa matibabu ya wanawake Dakta Job Obwaka, naibu mwenyekiti wa bodi ya hospitali hiyo Samson Kinyanjui, mkurugenzi Valery Gaya na mkurugenzi wa zamani Chris Bichage.
Kukamatwa kwao kumekosolewa na mawakili na usimamizi wa muungano wa madaktari, KMPDU.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 























































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































