SIASA MBAYA MAISHA MBAYA
Zaidi ya shilingi bilioni 608 hupotea kila mwaka humu nchini kupitia uifisadi, mwingiliano wa kisiasa ukitajwa kuwa kikwazo kikubwa katika kutoa haki kwenye kesi mbali mbali za ufisadi.
Haya ni kulingana na ripoti ya shirika la Transparency International, mkurugenzi mkuu wa shirika hilo Shilla Masinde akisema kesi nyingi zimekosa kuendelea kutokana na mwingiliano wa wanasiasa.
Nayo tume ya maadili na kukabili ufisadi EACC imesema licha ya kuwepo kwa sheria za kutosha za kukabili ufisadi, zimekuwa zikipuziliwa mbali.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 

























































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































