MGOMO WA WAHADHIRI WAANZA
Shughuli za masomo katika vyuo vikuu vya umma nchini zinatarajiwa kusambaratika kuanzia leo kufuatia mgomo wa wahadhiri ambao umenza rasmi usiku wa manane baada ya makataa yao kwa serikali kukamilika.
Katibu mkuu wa muungano wao UASU Dakta Constantine Wasonga, amesema juhudi zao kufanya mazungumzo na serikali zimefeli, mwenzake wa KUSU Charles Mukhwana, akisema hawatarejea kazini bila malalamishi yao kuangaziwa.
Hata hivyo, Waziri wa elimu Julius Ogamba, amesema juhudi zinaendelea kusitisha mgomo huo.
Imetayarishwa na Antony Ngongesa
English 

























































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































