#Local News

HUDUMA ZA AFYA ZATATIZIKA HOSPITALI YA MAMA LUCY

Huduma za afya katika hospitali ya mama Lucy katika kaunti ya Nairobi zimetatizika kufuatia mgomo wa matabibu na madaktari wa Kaunti huku madaktari wanafunzi wakiachwa kushughulikia Wagonjwa.

Chama cha matabibu nchini kimesisitiza kuwa wanachama wake hawatarudi kazini hadi pale madai yao yatakaposikilizwa na Serikali ambayo ni Pamoja na kulipwa kwa malimbikizi ya mishahara ya miezi kumi na tisa.

Chama hicho kimeitwa kwa mkutano na baraza la magavana ili kuweza kutafuta suluhu kwa Mgomo huo.

Imetayarishwa na Cyrus Sifuna

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *