LINDA MWANANCHI YATAKA POLISI WALIOWAVURUGA KUKAMATWA
Viongozi wa chama cha ODM wanaoegemea mrengo wa Linda Mwannchi, wametaka hatua mwafaka kuchukuliwa dhidi ya maafisa wa polisi waliowarushia viongozi hao vitoza machozi na kuvuruga mkutano wao mjini Narok hapo jana.
Wakiongozwa na seneta wa Nairobi Edwin Sifuna, mwenzake wa Vihiga Godfrey Osotsi, gavana wa Siaya James Orengo, na mbunge wa Embakasi East Babu Owino, viongozi hao wamewashutumu polisi kwa madai ya kuendelea kuwahangaisha, hatua wanayoitaja kuwa ukiukaji wa haki za kidemokrasia.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 

























































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































