#Local News

KINDIKI ATOA UJUMBE WA UMOJA WANAPOADHIMISHA PASAKA

Naibu Rais, Kithure Kindiki, amewahimiza Wakenya kujitafakari, kudumisha umoja na kujirekebisha wakati wa kipindi cha Pasaka, akieleza kuwa kujitoa kwa Yesu Kristo ni kielelezo cha hali ya juu cha upendo.

Katika ujumbe wa Ijumaa Kuu, Kindiki amesema Pasaka inaonyesha mfano mkubwa zaidi wa upendo kuwahi kushuhudiwa, akisisitiza umuhimu wa kipindi hicho katika kalenda ya Wakristo.

Ameongeza kuwa Pasaka ni fursa ya matumaini na ukombozi, akibainisha kuwa ni kipindi muhimu katika safari ya kiroho ya waumini.

Imetayarishwa na Cyrus Sifuna

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *