HAKUNA KUFICHA SURA, MAHAKAMA YAAMURU POLISI
Mahakama kuu imetoa amri ya kumwagiza Inspketa mkuu wa polisi kuhakikisha kwamba maafisa wa polisi wanaotumwa kuwashughulikia waandamanaji hawafichi nyuso zao mbali na kuhakikisha wanavalia sare zao zikionyesha majina na nambari zao za kazi.
Hii ni baada ya chama cha wansheria LSK kuwasilisha kesi mahakamani kikishikilia kwamba idara ya polisi inapanga njama ya kubuni kikosi cha siri.
Kulingana na Rais wa LSK Faith Odhiambo, maafisa wa polisi waliowajeruhi waandamanaji wanafaa kuwajibishwa.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 

























































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































